Viongozi Afrika washinikiza mageuzi katika mifumo ya mikopo
12 Mei 2026
Zaidi ya viongozi 30 wa serikali za Afrika wanahudhuria mkutano huo unaofanyika jijini Nairobi, Kenya, unaoitwa Africa Forward—ikiwa ni mara ya kwanza kwa Ufaransa kuandaa mkutano wa aina hiyo katika nchi ya Afrika inayozungumza Kiingereza.
Rais wa Kenya William Ruto amesema, "Sisi kama viongozi wa Afrika tunaelewa kwamba pia tuna wajibu wetu. Uhusiano huu hauwezi kuwa wa upande mmoja. Tunatarajia kutoka kwa Ufaransa kama ambavyo wao watatarajia kutoka kwetu, na wao watatoa kadiri tunavyotoa sisi. Huo ndiyo ushindi wa kweli kwa pande zote - uhusiano wa manufaa ya pamoja."
Macron ameusifu mkutano huo, akisema umechochea ahadi za uwekezaji wa euro bilioni 23 barani Afrika, akitaja hatua hiyo kama ushahidi wa dhamira ya Ufaransa kujenga uhusiano wa usawa na mataifa ya bara hilo.