Mazungumzo ya wiki mbili ya kuutatua mgogoro wa Libya yaliyofanyika nchini Tunisia ambayo yalidhaminiwa na Umoja wa Mataifa yamemalizika bila ya mafanikio. Je lini kutapatikana muafaka nchini humo? Hilo ni swali linalojibiwa na na mchambuzi wa masuala ya kisiasa Ahmed Rajabu akigusia pia juu ya mustakabali wa taifa hilo la afrika ya kaskazini.