Umoja wa Mataifa waonya kuhusu hali Sudan Kusini
26 Januari 2026
Taarifa iliyotolewa Jumapili na tume hiyo imeelezea hofu kubwa kutokana na mapigano yanayoendelea huko Jonglei, Kaskazini mwa Juba. Kulingana na ripoti hiyo, mashuhuda kwenye eneo hilo wamesema walishuhudia raia wakikimbilia kujificha kwenye madimbwi yenye maji mengi.
Makamanda wa jeshi wadaiwa kuchochea ghasia dhidi ya raia
Tume hiyo imesema taarifa kwa umma zilizotolewa na makamanda zinazohimiza ghasia dhidi ya raia pamoja na kuwaandaa wanajeshi zinaakisi uchochezi hatari wakati ambapo misingi ya mchakato wa amani tayari imeshadhoofika Sudan Kusini.
Taifa hilo changa zaidi duniani limekuwa likikabiliwa na vita, umasikini na ufisadi mkubwa tangu lilipoanzishwa mwaka 2011. Makubaliano ya kugawana madaraka kati ya Rais Salva Kiir na msaidizi wake Riek Machar yaliingia dosari baada ya Machar kutiwa mbaroni ambapo anakabiliwa na kesi ya uhalifu dhidi ya ubinadamu.