Ukraine yashambulia kituo cha kusafisha mafuta cha Urusi
20 Aprili 2026
Maafisa wa Urusi wamesema shambulio la droni la Ukraine dhidi ya bandari ya Tuapse katika bahari nyeusi limesababisha moto mkubwa na kifo cha mtu mmoja, kabla ya moto huo kudhibitiwa saa chache baadae.
Gavana wa eneo hilo la Tuapse Veniamin Kondratiev, amesema shambulio hilo limefanya uharibifu mkubwa ndani dhidi ya majengo kadhaa kote mjini humo ikiwa ni pamoja na shule ya msingi, majengo ya makazi, chekechea, jumba la makumbusho na kanisa.
Wizara ya ulinzi ya Urusi pia imeripoti kudungua droni 112 za Ukraine usiku wa kuamkia leo.
Katika hatua nyingine, Urusi imesema leo kuwa imemkamata mwanamke mmoja raia wa Ujerumani aliyepatikana na bomu la kujitengenezea, kwenye mkoba wake katika kile kinachodaiwa kuwa njama iliyopangwa na Ukraine ya kulipua kituo kimoja cha usalama kusini mwa nchi hiyo.
Urusi imewakamata watu kadhaa katika vita vyake vya miaka minne nchini Ukraine, wengi wao raia wake yenyewe, kwa madai ya kuifanyia kazi Ukraine.