1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tunisia yatoa hukumu ya kifo juu ya chapisho la Facebook

4 Oktoba 2025

Mahakama moja nchini Tunisia imemhukumu kifo mwanamume wa umri wa miaka 51 kuhusiana na chapisho katika mtandao wa Facebook lililoonekana kumkera Rais wa nchi hiyo Kais Saied.

https://p.dw.com/p/51UE2
Ubelgiji  Brüssel 2025 | Appu za mitandao ya kijamii
Picha za kwenye simu za appu za mitandao ya kijamii Picha: Jonathan Raa/NurPhoto/picture alliance

Katika taarifa kwenye Facebook, Bouthelja amesema kuwa mteja wake ambaye hakutajwa jina, alikuwa kizuizini tangu Januari 2024, kabla ya kesi kuanza. Amesema mshtakiwa ni baba wa watoto watatu na mfanyakazi wa kutwa anayeishi na ulemavu uliosababishwa na ajali iliyotokea kazini mwake.

Mshtakiwa hana ushawishi mkubwa wa mitandao

Bouthelja amesema mteja wake ana kiwango duni cha elimu na asiyekuwa na ushawishi mkubwa mtandaoni.

Uamuzi huo ni wa hivi karibuni zaidi kutumia Amri ya 54, sheria inayoifanya haramu kutayarisha, kueneza, kusambaza, kutuma au kuandika habari za uongo kwa lengo la kukiuka haki za wengine, kudhuru usalama wa umma au ulinzi wa taifa au kuzusha hofu miongoni mwa watu.