1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tanzania: Tume ya Jaji Chande yawasilisha ripoti yake

23 Aprili 2026

Ripoti ya Tume ya uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, 2025 nchini Tanzania imewasilishwa Alhamisi, katika mkutano uliohudhuriwa na Rais wa nchi hiyo Samia Suluhu Hassan.

https://p.dw.com/p/5Chxk
Tume ya uchunguzi wa matukio ya kabla na baada ya uchaguzi wa Oktoba 2025 imewasilisha ripoti yake.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya kabla na baada ya uchaguzi wa Oktoba 2025 Picha: Commission of Inquiry Tanzania

Miongoni mwa mambo makuu yaliyotangazwa na mkuu wa tume hiyo Jaji Mstaafu Mohammed Chande, ni kuwa idadi ya waliouawa wakati wa ghasia hizo ni 519, na waliojeruhiwa ni zaidi ya 2000.

Thamani ya mali zilizoharibiwa yatajwa

Aidha, thamani ya mali iliyoharibiwa ni shilingi bilioni 125 za Tanzania. Ingawa ripoti haikuelekeza lawama za wazi upande wowote, imesema kuhusu uwezekano wa kutokea kwa matumizi mabaya ya silaha na kutaka uchunguzi wa kina ufanyike.