1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sissi aapishwa kwa muhula wa tatu Misri

2 Aprili 2024

Rais Abdel Fattah al-Sissi wa Misri ataapishwa leo kwa muhula wa tatu madarakani katika majengo mapya ya bunge yaliojengwa nje ya mji mkuu, Kairo.

https://p.dw.com/p/4eKur
Rais Abdel-Fattah al-Sissi wa Misri
Rais Abdel-Fattah al-Sissi wa Misri anaapishwa kwa muhula wa tatu madarakani.Picha: John Macdougall/AP Photo/picture alliance

Al- Sissi mwenye umri wa miaka 69 na ambaye ameliongoza taifa hilo kwa zaidi ya muongo mmoja, ataanza rasmi muhula wake mpya hapo kesho, ikiwa ni zaidi ya miezi mitatu baada ya kuchaguliwa tena kama rais wa nchi hiyo kwa asilimia 89.6 za kura.

Mustafa Bakri, mbunge mwenye ushirikiano wa karibu na mamlaka nchini humo, amesema kulingana na katiba, muhula huu mpya wa miaka sita, unatarajiwa kuwa wa mwisho kwa uongozi wa Sissi.

Soma zaidi: Wamisri wanapiga kura leo kumchagua Rais

Mbunge huyo aliongeza kuwa huenda serikali ikajiuzulu baada ya kuapishwa kwaSissi kuruhusu kufanyika mabadiliko katika baraza la mawaziri.

Kuapishwa kwa Sissi kunakuja wakati ambapo taifa hilo linakabiliwa na mzozo mbaya wa kiuchumi, kuongezeka kwa mfumuko wa bei na uhaba wa sarafu za kigeni.

Lakini mwanzoni mwa mwaka huu, Misri ilipokea mikopo kutoka kwa Umoja wa Falme za Kiarabu na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF).