1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Saudi Arabia, Qatar na Oman yamshawishi Trump kuhusu Iran

15 Januari 2026

Saudi Arabia, Qatar na Oman zimeongoza juhudi za mazungumzo na Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu tishio la shambulizi dhidi ya Iran.

https://p.dw.com/p/56tJp
Marekani Washington D.C. 2026 | Donald Trump
Rais wa Marekani, Donlad TrumpPicha: Mandel Ngan/AFP/Getty Images

Afisa huyo aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina, amesema mataifa hayo matatu ya Ghuba yaliongoza juhudi pana za kidiplomasia za dakika za mwisho kumshawishi Trump kuipa Iran nafasi ya kuonyesha nia njema.

Amesema mazungumzo bado yanaendelea kudumisha imani iliyoko.

Katika hatua nyingine, Shirikisho la Kimataifa la Msalaba Mwekundu, limesema  kwamba afisa mmoja wa Shirika lake la Hilali Nyekundu Amir Ali Latifi ameuawa na wenzake wengine watano kujeruhiwa walipokuwa kazini mkoani Gilan kaskazini-magharibi mwa Iran mnamo Januari 10.

Haya ni kulingana na maelezo kupitia taarifa yake iliyotoa kutoka makao yake makuu huko Geneva, bila kutoa maelezo zaidi.