Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir ametangaza hali ya hatari katika jimbo la Bahr el Ghazal. Rais wa Venezuela Nicolas Maduro amepuuza vitisho vya Marekani kuiwekea nchi yake vikwazo kuhusu mpango wa kuandika upya katiba ya nchi. Kanisa Katoliki nchini Ujerumani limetikishwa na kashfa ya udhalilishaji wa kingono dhidi ya watoto wa kiume katika shule ya kwaya ya Regenburgs Domspatzen.