Rais wa Zanzibar, Dokta Hussen Mwinyi amesema hana wasiwasi wowote kuhusu majaliwa ya serikali ya Umoja wa Kitaifa iliyoundwa hivi karibuni. Akizungumza na George Njogopa wa DW, Rais Mwinyi ambaye leo anatimiza siku 100 madarakani, amedokeza matamanio yake kuhusu mwelekeo mpya wa kisiasa hasa baada ya kuundwa kwa serikali mpya ya Umoja wa Kitaifa inayovishirikisha vyama vya CCM na ACT-Wazalendo.