Aliyekuwa mwanasheria mkuu na mwandishi wa katiba ya sasa ya Zanzibar, Aboubakar Khamis Bakari, amefariki dunia, akikumbukwa kuwa mmoja wa mihimili mikubwa ya kisheria na kiutawala kwenye visiwa hivyo vya Bahari ya Hindi, ambavyo kwa muda mrefu vimekuwa kwenye misukosuko ya kisiasa. Mohammed Khelef amezungumza na mwanasheria mkuu mwenzake wa zamani, Othman Masoud, juu ya maisha yake.