1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu sita walijeruhiwa na watatu kati yao vibaya

Deo Kaji Makomba
19 Agosti 2020

Waendesha mashitaka mjini Berlin wanasema huenda mashambulizi yaliyofanywa na mtu mwenye umri wa miaka 30 raia wa Iraq huko katika barabara kuu mjini Berlin hivi leo yanatokana na imani kali ya kidini.

https://p.dw.com/p/3hBe6
Berlin Unfälle auf A100
Moja ya gari lililotumika katika shambulio mjini BerlinPicha: picture-alliance/dpa/P. Zinken

Watu sita walijeruhiwa na watatu kati yao vibaya, wakati mtu huyo inadaiwa aliendesha gari kadhaa Jumanne jioni na kunyoosha kwenye barabara kuu ya mji mkuu wa Ujerumani, Berlin. Ofisi ya mwendesha mashitaka ziliarifu kuwa kulingana na hali ya uchunguzi wao tukio hilo lilikuwa ni shambulio lililochochewa na mtu mwenye imani kali.

Mfululizo wa mashambulio ulisababisha kufungwa kwa moja ya njia muhimu ya usafiri katika mji wa Berlin. Pia kulikuwa na dalili kwamba mtu huyo alikuwa akiugua matatizo ya kisaikolojia, Shirika la habari la Ujeruman, dpa, liliripoti.

Polisi na waendesha mashitaka bado hawajaweka bayana nini ilikuwa nia ya dereva huyo, lakini dpa liliripoti kwamba wachunguzi wanaangalia ikiwa mtu huyo alitenda kwasababu za kisiasa au kama alikuwa mgonjwa wa akili.

Wakati hayo yakitokea, jeshi la polisi mjini Berlin lilisema kuwa mtu huyo alisababisha ajali tatu katika vituo vitatu vya tren 100 katika mji wa Tempelhof-Schoeneberg wa jiji hilo kabla ya kudai kwamba sanduku kwenye gari lake lilikuwa na kitu hatari.

Hata hivyo wakati polisi walifungua sanduku kwa kutumia ndege za maji zenye shinikizo kubwa iligundulika kuwa haina zana yoyote ya hatari. Dereva alikamatwa na barabara ilifungwa kwa masaa kadhaa, na kusababisha usumbufu mkubwa wa kusafiri.

Vyombo vya habari vya Ujerumani viliripoti kwamba dereva wa pikipiki alikuwa mmoja wa wale waliojeruhiwa.

Watu waliofungamana na msimamo mkali wa Kiislamu wamefanya mashambulio kadhaa ya vurugu nchini Ujerumani katika miaka ya hivi karibuni.

Chanzo: dpa/AFP