Marekani yaendeleza juhudi ya kumtafuta rubani wake
4 Aprili 2026
Matangazo
Ndege hiyo ya Marekani, iliyotambuliwa na Iran kuwa F-15E, ilikuwa mojawapo ya ndege mbili zilizoshambuliwa jana Ijumaa, huku rubani mmoja akiokolewa na mwingine kutoweka.
Hii ni mara ya kwanza kwa Marekani kupoteza ndege katika ardhi ya Iran tangu kuanza kwa vita hivyo ambavyo vimeingia sasa wiki yake ya sita, hatua inayoweza kuashiria mabadiliko katika mwwelekeo wa vita hivyo.
Kwengineko shirika la atomiki la Iran limesema shambulizi la anga limelenga karibu na kituo chake cha nyuklia cha Bushehr, na kuua mlinzi mmoja na pia kuharibu jengo lingine la karibu. Shirika hilo limetangaza hayo kupitia chapisho kwenye mitandao ya kijamii. Hii ni mara ya nne kwa kituo hicho kulengwa wakati wa vita.