Jumatatu ya wiki inayomalizika, Kansela wa Ujerumani Angela Merkel alitangaza kwamba hatagombea tena uongozi wa chama chake cha CDU mwezi ujao wa Desemba, na kwamba muhula wake huu wa nne ni wa mwisho. Wanasiasa mbali mbali wanajipanga kuchukua nafasi yake. Katika makala hii ya Maoni kwenye Meza Duara, washiriki wanajadilin hali ya Ujerumani baada ya uongozi wa muda mrefu wa Kansela Angela Merkel.