Kenya inajiandaa kufanya uchaguzi mkuu tarehe nane Agosti. Wakenya milioni 19.6 wanatarajiwa kujitokeza katika vituo 40,883, kupiga kura zao kuwachagua viongozi wao, akiwemo rais, gavana, mbunge, seneta, muwakilishi wa bunge la kaunti na muwaskilishi wa wanawake. Tume ya uchaguzi na mipaka IEBC inasema iko tayari kabisa kwa uchaguzi huo mkuu, licha ya dalili kuonesha inasuasua.