1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kremlin yamshtumu Zelensky juu ya Siku ya Ushindi

9 Mei 2026

Urusi imetoa jibu fupi na la wazi kwa amri ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ya "kuidhinisha" gwaride la kijeshi la Mei 9 mjini Moscow baada ya siku kadhaa za uvumi kwamba hafla hiyo inaweza kushambuliwa.

https://p.dw.com/p/5DWKi
Dmitry Peskov
Msemaji wa ikulu ya kremlin Dmitry PeskovPicha: Alexander Kazakov/TASS/ZUMA/picture alliance

Kabla ya sherehe hiyo ya leo ya Siku ya Ushindi ya uliokuwa Umoja wa Kisovieti dhidi ya utawala wa Kinazi wa Ujerumani katika Vita vya Pili vya Dunia, msemaji wa ikulu ya Kremlin Dmitry Peskov, ameiambia televisheni ya serikali ya Urusi kwamba hawahitaji ruhusa ya mtu yeyote kuandaa sherehe hizo.

Peskov ametoa onyo kwa yeyote atakayejaribu kudhihaki na kufanya utani kuhusu siku hiyo.

Ameongeza kusema kuwa "Siku ya Ushindi"inaadhimishwa katika sehemu kubwa za uliokuwa Umoja huo wa Kisovieti kama "siku ya fahari na machozi," na kwamba Umoja huo ambao sasa umevunjika na ambao pia uliijumuisha Ukraine, ulipoteza zaidi ya watu milioni 27 wakati wa ukombozi wa Ulaya kutoka kwa dikteta wa Ujerumani Adolf Hitler.