Kenya iliishinda Djibouti Alhamisi (18.06.20209 kuchukua kiti cha mwisho cha bara la Afrika katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa. Kenya ilipata kura 129 dhidi ya kura 62 za Djibouti katika duru ya pili ya uchaguzi kujiunga na Tunisia na Niger katika baraza hilo kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia (01.01.2021) ikichukua mahala pa Afrika Kusini.