Joseph Kabila ahukumiwa kifo kwa uhaini
1 Oktoba 2025
Matangazo
Hukumu hiyo imetolewa jana Jumanne na Luteni Jenerali Joseph Mutombo Katalayi mjini Kinshasa bila ya yeye mwenyewe kuwepo.
Kabila alipatikana na hatia ya kushirikiana na kundi la waasi la M23 linaloipinga serikali, na ambalo limeteka maeneo mengi ya mashariki mwa Kongo yenye utajiri mkubwa wa rasilimali wakisaidiwa na Rwanda.
Aliondoka nchini humo mwaka 2023 na kuonekana tena mwezi Mei mwaka huu katika mji wa Goma unaokaliwa na waasi hao hatua iliyoibua wasiwasi mjini Kinshasa.
Wafuatiliaji wa mambo wanasema hukumu hiyo inalenga tu kuzuia azma yake ya kuunganisha upinzani, licha ya kwamba hajulikani aliko kwa sasa.