1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
BiasharaJapan

Japan yaikamata meli ya China na kuongeza uhasama baina yao

13 Februari 2026

Japan imeikamata meli ya uvuvi ya China na kumshikilia nahodha wa meli hiyo madai ya kukimbia ukaguzi wakati ilipokuwa kwenye ukanda wake maalumu wa kiuchumi, hatua inayoongeza mivutano baina ya mataifa hayo mawili.

https://p.dw.com/p/58flY
Japan Tokyo 2025 | Maafisa kutoka Kikosi cha Walinzi wa Pwani cha Japan wakiingia kwenye meli waliyoitilia shaka kama sehemu ya mafunzo kwenye bandari ya Tokyo
Japan imeikamata meli ya uvuvi ya China kwa madai ilipuuza amri ya kusimama ili kukaguliwa, hatua iliyochochea mzozo baina ya nchi hizo.Picha: Kazuhiro Nogi/AFP

Taasisi ya Uvuvi ya Japan imethibitisha kuikamata meli hiyo na kusema nahodha aliamriwa kusimama kwa ajili ya kukaguliwa na wakaguzi wa uvuvi, lakini alipuuza amri hiyo.

Meli hiyo ilikuwa na watu kumi pamoja na nahodha.

Ingawa Japan ikiwa ilizikamata meli za Korea Kusini na Taiwan katika miaka ya karibuni, lakini kisa hiki ni cha kwanza kinachohusisha meli kutoka China, tangu mwaka 2022.

Na ni kisa kinachojitokeza katikati ya mvutano wa kidiplomasia kati ya China na Japan, ulioanza mwezi Novemba baada ya kiongozi mpya wa Japan mhafidhina Sanae Takaichi kuashiria kwamba shambulizi lolote dhidi yao linaweza kuchochea hatua ya kijeshi.