Gaza na Palestina kujadiliwa kwenye mkutano wa UN
20 Septemba 2025
Matangazo
Kwa kukiuka taratibu, Baraza hilo Kuu jana lilipiga kura ya kumruhusu Abbas kuhutubia mkutano huo kwa njia ya video huku akiwakilishwa katika mkutano huo na balozi wa Palestina kwenye Umoja wa Mataifa.
Maafa ya kibinadamu yanayolikumba eneo la Gaza yatakuwa kipaumbele cha mkutano huo, miaka miwili baada ya kuanza kwa mashambulizi ya Israel katika Ukanda wa Gaza yaliochochewa na shambulio la Hamas mnamo Oktoba 7, 2023.
Kuanzia Jumatatu, Saudi Arabia na Ufaransa zitaongoza kwa pamoja mikutano kuhusu suluhu la mataifa mawili ya Israel na Palestina, inayolenga kuona pande hizo mbili zikishirikiana kwa amani.