Faru huyo pekee wa kiume duniani kwa jina Sudan amefariki nchini Kenya kutokana na matatizo ya kiafya ya uzee. Watafiti wamevuna jeni zake ili kujaribu kutumia siku za usoni kutungisha mayai kutoka kwa faru wawili pekee wa kike waliosalia duniani kwa njia ya teknolojia ili kuendeleza kizazi cha faru hao aina ya 'Nothern White Rhino'.