Ethiopia yakabiliwa na hatari ya kukosa chakula cha msaada
10 Oktoba 2025
Matangazo
Mkurugenzi wa shirika hilo la WFP nchini Ethiopia, Zlatan Milisic, amesema linahitaji kukusanya takriban dola milioni 230 kuendeleza shughuli za kibinadamu kwa muda wa miezi sita ijayo.
Katika taarifa, Milisic amesema kuwa bila ya ufadhili mpya wa haraka, WFP inaweza kulazimika kusitisha kabisa msaada wa chakula kwa wakimbizi wote nchini Ethiopia katika miezi ijayo.
WFP yalazimika kupunguza mgao wa chakula
Mwezi huu, WFP ililazimika kupunguza mgao wa chakula kwa wakimbizi 780,000 katika kambi 27 kote Ethiopia.
Milisic amesema wanafanya maamuzi yasiowezekana.
Ameongeza kuwa mapunguzo hayo ni hatua nyingine ya kuelekea kusimamisha kabisa usambazaji wa chakula na kuweka maisha ya wale wanaopata msaada kwa sasa kuwa katika hali ya hatari.