1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China yasema inataka uhusiano wa ngazi mpya na Ujerumani

15 Februari 2026

Mwanadiplomasia mkuu wa China Wang Yi amemwambia Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz kwamba Beijing inatumai kuimarisha uhusiano wa pande mbili kufikia "ngazi mpya".

https://p.dw.com/p/58nRe
Munich 2026 | Friedrich Merz na Wang Yi
Waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi (kushoto) na waziri mkuu wa Ujerumani Friedrich Merz ( kulia)Picha: Michael Bihlmayer/CHROMORANGE/picture alliance

Kwa mujibu wa taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya China, Wang pia amemwambia Merz kwamba China inatarajia kufanya kazi na Ujerumani kuleta "ushirikiano wa kimkakati wa pande zote".

Ameongeza kuwa kwa msaada wa Ujerumani, China pia inataka kujiandaa kwa hatua inayofuata ya ushirikiano wa ngazi za juu.

Wang amethibitisha kuiunga mkono Ujerumani kuchukua jukumu kubwa zaidi katika kudumisha "uhuru wake wa kimkakati na kujitegemea na kuwa nguvu ya kuleta ushirikiano kati ya China na mataifa ya Ulaya.

Merz anaripotiwa kujiandaa kufanya ziara yake ya kwanza nchini China mwezi huu, huku suala kuu likiwa ni jinsi ya kushughulikia mahusiano ya kibiashara yanayoendelea kubadilika.