Rais wa China Xi Jinping ameahidi kutoa kiasi cha dola bilioni 60 kwa ajili ya maendeleo ya Afrika katika kipindi cha miaka mitatu ijayo. Ufadhili huo utajumlisha dola bilioni 15 za msaada wa bure na mikopo isiyo na riba, katika juhudi za kutuliza wasiwasi kwamba msaada wa China unazidi kuyatumbukiza mataifa ya Afrika katika madeni.