SiasaThailand
Bunge la Thailand lavunjwa kwa ajili ya uchaguzi mpya
12 Desemba 2025
Matangazo
Waziri Mkuu Anutin aliyedumu madarakani kwa takribani miezi minne, amelivunja Baraza la Wawakilishi baada ya kupewa idhini na Mfalme Maha Vajiralongkorn.
Kwenye mkutano na waandishi wa habari mapema leo mjini Bangkok, Anutin alisema uamuzi huo ulitokana na hatua ya chama kikuu cha upinzani cha People kuondoa uungaji wake mkono bungeni.
Ni hatua inayochukuliwa huku kukiwa na kipindi kigumu cha kisiasa, kinachoshuhudia mapigano makali kati ya Thailand na Cambodia ambapo maelfu ya watu pande zote mbili za mpaka wanayakimbia makaazi yao.