Australia yavunja mtandao wa 'kishetani' dhidi ya watoto
1 Desemba 2025
Matangazo
Polisi nchini Australia imesema siku ya Jumatatu kuwa imewashitaki watu wanne mjini Sydney, wanaoshukiwa kuwa sehemu ya mtandao wa kimataifa unaosambaza kile ilichokiita maudhui ya ‘kishetani' ya unyanyasaji wa watoto kingono.
Kulingana na taarifa ya polisi jimbo la New South Wales, maafisa wao waliwakamata watuhumiwa hao baada ya kuchunguza kadhia hiyo ya kimataifa dhidi ya watoto.
Wakati wa uchunguzi, wapelelezi walifichua mtandao wa wanyanyasaji watoto kingono wanaohusika pakubwa katika kumiliki, kusambaza na kuwezesha uwepo wa maudhui hayo kwenye tovuti inayosimamiwa kimataifa.