WHO yapandisha tahadhari ya hatari ya Ebola nchini Kongo
22 Mei 2026
Matangazo
Shirika la Afya Duniani, WHO, limesema hatari ya kiafya kwa umma kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imeongezwa kwa kiwango cha juu zaidi.
Hata hivyo, Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus, amesema kuwa, kiwango cha hatari kinasalia kuwa cha juu katika ngazi ya kikanda na cha chini katika ngazi ya dunia. Alitoa kauli hiyo Ijumaa katika mkutano na wanahabari.
Kwa mujibu wa WHO, kwa sasa kuna karibu visa 750 vinavyoshukiwa kuwa vya Ebola nchini Kongo, huku vifo vinavyohusishwa na ugonjwa huo vikifikia 177.
Wakati huo pia hofu imezidi kutanda baada ya mlipuko wa Ebola kuenea hadi jimbo la Kivu Kusini mashariki mwa Congo eneo linalodhibitiwa na waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda.