Mashirika ya kutetea Haki za Binadamu nchini Kenya yamevikosoa vyombo vya dola kwa jinsi vinavyotekeleza amri ya kutotoka nje usiku baada ya mauaji ya mtoto wa miaka 13 Jumatatu usiku. Wazazi wa mtoto huyo wanataka haki itendeke dhidi ya maafisa waliohusika.