Viongozi wa China wasusia mkutano wa ulinzi Singapore
29 Mei 2026
Matangazo
Maafisa wakuu wa China hawatakuwepo katika mkutano huo wa siku tatu, ambao utajadili masuala muhimu kama mgogoro wa Taiwan na Beijing pamoja na vita vya Iran.
Hii ni mara ya pili kwa Waziri wa Ulinzi wa China Dong Jun, kutoshiriki mkutano huo unaowaleta pamoja maafisa wa ulinzi kutoka mataifa 45. Hii inamaanisha Jun hatokuwa na mkutano na Hegseth wakati ambapo China imetoa onyo kali kwa Marekani kwamba iwe makini kwa namna inavyoishughulikia Taiwan.
Hivi karibuni Rais Donald Trump alifanya ziara ya siku mbili Chini akitaka nchi hiyo iisaidie kuishinikiza Iran kufungua njia ya bahari ya Hormuz.
China inazingatia kisiwa cha Taiwan kinachojitawala chenyewe kuwa sehemu ya eneo lake.