Hali ya usalama nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inazidi kuwa ya wasiwasi kutokana na mashambulizi yanayofanywa na waasi. Duru zinasema majeshi ya usalama mwishoni mwa juma yaliwaua washambuliaji 31 waliokuwa na silaha mjini Lubumbashi ambao ni wafuasi wa mbabe wa zamani wa kivita Gedeon Kyungu Mutanga. Sikiliza mahojiano kati wenzetu Sylvia Mwehozi na Saleh Mwanamilongo.