Licha ya ukosolewaji dhidi ya hatua za kushitukiza zinazochukuliwa na Rais John Magufuli wa Tanzania kwenye sekta ya uchumi na utawala, Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Geoffrey Mwambe, anasema ukweli ni kuwa hatua hizo zinawafurahisha na kuwanufaisha wawekezaji walio wengi na kwamba zimeanza kuleta manufaa kwa nchi. Msikilize akizungumza na Mohammed Khelef.