1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sudan yaipongeza hatua ya Pompeo

3 Agosti 2020

Sudan yapongeza matamshi ya Pompeo kuhusu kuiondoa katika orodha ya ugaidi

https://p.dw.com/p/3gKXh
USA Mike Pompeo
Picha: picture-alliance/ZUMAPRESS.com/R. Chiu

Vyombo vya habari nchini Sudan vinasema serikali nchini humo imefurahishwa na matamshi ya Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo kwamba anataka kuiondoa Sudan kutoka kwenye orodha ya wafadhili wa ugaidi.

Pompeo ametoa kauli hiyo mara kadhaa kwani kuiweka Sudan kwenye orodha hiyo ni jambo linalozuia uwekezaji katika nchi hiyo. Lakini kuna kutoelewana kuhusiana na kiwango cha fidia itakayotolewa kutokana na mashambulizi ya mabomu ya balozi mbili za Marekani.

Pompeo ameiambia kamati ya mambo ya nje ya baraza la seneti la Marekani kuwa maelewano yatafikiwa hivi karibuni na kuwasilishwa mbele ya bunge. Serikali ya Sudan kwa upande wake imesema itachukua hatua zote ili kutimiza vigezo vya Marekani vitakavyosaidia maamuzi kwenda upande wao.