MigogoroUkraine
Starmer ataka mzozo wa Ukraine usisahauliwe
18 Machi 2026
Matangazo
Starmer alisema hayo alipomkaribisha Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy kwenye makazi na ofisi yake, kwenye mtaa wa Downing, jijini London na kuongeza kuwa hawapaswi kupoteza mwelekeo kuhusu kinachoendelea Ukraine na hasa msaada wao kwa taifa hilo.
Zelenskyy alimpa Starmer taarifa kuhusu kile kinachoendelea kwenye vita vyake na Urusi, usalama wa nishati, na juhudi zinazoendelea za kidiplomasia na Marekani na Urusi.
Katibu Mkuu wa NATO Mark Rutte pia alijiunga na mkutano huo na kufanya mazungumzo tofauti na Zelenskyy.