1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shinikizo lazidi kumuelemea Xabi Alonso

11 Desemba 2025

Kocha wa Real Madrid Xabi Alonso amewashukuru wachezaji wake kwa kujituma uwanjani licha ya kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Manchester City katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyochezwa kwenye uga wa Santiago.

https://p.dw.com/p/557Y2
Soka la Bundesliga | Xabi Alonso akiwaaga mashabiki wa Bayer Leverkusen katika mchezo wake wa mwisho wa nyumbani
Kocha wa zamani wa Leverkusen Xabi Alonso akiwaaga mashabiki baada ya mchezo wake wa mwisho wa nyumbani, na kuelekea Real MadridPicha: Marius Becker/dpa/picture alliance

Alonso amesema anaamini klabu hiyo itarejea kwenye kiwango chake cha kawaida hivi karibuni. Miamba hao wa Uhispania wamepata ushindi katika mechi mbili tu kati ya nane zilizopita katika mashindano yote.

Matokeo hayo yameongeza shinikizo kwa Alonso huku vyombo vya habari nchini humo vikiripoti juu ya kuwepo kwa mvutano kati ya kocha huyo na baadhi ya wachezaji, ingawa baadhi wamejitokeza hadharani na kuonyesha kumuunga mkono.

Mpambano kati ya Madrid na City ndio ulikuwa mkali zaidi wa raundi hiyo katikati ya ripoti kwamba Alonso alikuwa anakabiliwa na kitisho cha kupoteza udhibiti wa wachezaji wake, hali inayoongeza uvumi kuhusiana na kuendelea kusalia kwenye nafasi yake.

Kulishuhudiwa vijembe na kejeli ndani ya Bernabeu baada ya filimbi ya mwisho kulia.

Ligi ya Mabingwa ya UEFA 2025 | Real Madrid dhidi ya Manchester City | Rodrygo Goes asherehekea bao lake
Rodrygo Goes, Winga wa kulia wa Real Madrid na Brazil akisherehekea baada ya kuifungia timu yake bao la kwanza wakati wa mechi ya Ligi ya Mabingwa ya UEFA 2025/26 dhidi ya Manchester City katika Uwanja wa Estadio Santiago Bernabeu Disemba 10, 2025.Picha: Jose Breton/NurPhoto/picture alliance

"Tunajua ni wakati mgumu kwetu na kwa kocha," winga wa Madrid Rodrygo alisema. "Mambo hayaendi kama tunavyotaka na nilitaka kuonyesha kwamba tuko nyuma ya kocha wetu. Nilitaka kuonyesha. kwamba tuko pamoja na tunahitaji kuwa na umoja ili kuendelea kusonga mbele na kufikia malengo yetu."

Klabu ya Arsenal inaendelea kushika kasi katika mashindano ya msimu huu hasa baada ya ushindi wa 3-0 dhidi ya Club Brugge, huku bingwa mtetezi Paris Saint-Germain ikimaliza bila ya kufungana na Athletic Bilbao.

Kwingineko, klabu inayoshiriki ligi kuu ya Ujerumani Bundesliga, Bayer Leverkusen imetoka sare ya 2-2 na Newcastle United katika mchezo wa kusisimua wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Alejandro Grimaldo alifunga bao dakika ya 88 ya mchezo na kuhakikisha wanagawana alama na Newcastle.