Senegal yatangaza kuandaa uchaguzi haraka iwezekanavyo
17 Februari 2024Matangazo
Msemaji wa Rais Sally, Yoro Dia, amesema kuwa rais anakusudia kutii maamuzi hayo ya Baraza la Katiba ambalo lilisema hapo jana kuwa kuuchelewesha uchaguzi huo uliopangwa mnamo Februari 25 hadi Desemba 15, ni kinyume na katiba. Hata hivyo msemaji huyo hakutaja tarehe mpya ya uchaguzi.
Soma pia:Serikali ya Senegal yasaka suluhu ya mzozo wa kuahirisha uchaguzi
Senegal ilichukuliwa kuwa mojawapo ya nchi zenye demokrasia thabiti katika eneo la Afrika magharibi ambalo limeshuhudia mkururo wa mapinduzi ya kijeshi, lakini misuguano kuhusu uchaguzi wa mwaka huu imelitumbukiza taifa hilo kwenye mzozo wa kisiasa, ikiwemo kufanyika maandamano ya ghasia yaliosababisha vifo vya watu watatu na wengine kadhaa wakiwemo maafisa usalama kujeruhiwa.