Bolsonaro miaka 27 jela kwa jaribio la kuipindua serikali
12 Septemba 2025
Matangazo
Bolsonaro, ambae mara zote amekuwa akikataa kuhusika na maovu ya aina yoyote anaweza kuukatia rufaa uamuzi uliotolewa. Kwa sasa yuko katika kifungo cha nyumbani mjini Brasilia.
Majaji wanne kati ya watano waliokuwa wakipitia kesi kesi yake walimkuta na hatia kwa makosa matano, uamuzi utakaozidisha migawanyiko ya kisiasa.
Makosa hayo ni pamoja na kujaribu kufanya mapinduzi baada ya kushindwa uchaguzi 2022, mipango ya kumuua rais wa sasa Luiz Inácio Lula da Silva, kushiriki katika genge la wahalifu, kujaribu kuvuruga utawala wa sheria pamoja na kuzua vurugu.
Bolsonaro ndio rais wa kwanza wa Brazil kuhukumiwa kwa jaribio la mapinduzi.