1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais Rajoelina adaiwa kukimbilia kusikojulikana

13 Oktoba 2025

Kufuatia shinikizo la maandamano ya vijana wakiungwa mkono na jeshi, rais Andry Rajoelina yadaiwa ameikimbia nchi

https://p.dw.com/p/51uvr
Rais Andry Rajoelina akabiliwa na shinikizo kubwa la maandamano ya kupinga uongozi wake
Rais Andry Rajoelina akabiliwa na shinikizo kubwa la maandamano ya kupinga uongozi wake Picha: Siphiwe Sibeko/REUTERS

Kiongozi wa upinzani nchini Madagascar, Siteny Randrianasoloniaiko amesema rais Andry Rajoelina ameikimbia nchi.

Kiongozi huyo wa upinzani ameliambia  shirika la habari la Reuters hivi leo kwamba taarifa za kuondoka nchini, Rajoelina zimaethibitishwa na wafanyakazi wa ofisi ya rais.

Hata hivyo msemaji wa rais hakupatikana mara moja kutowa tamko kuhusu taarifa hiyo, alipotafutwa na shirika la habari la Ufaransa, RFI.

Kiongozi wa upinzani Randrianasoloniaiko amesema raisAndry Rajoelinahajulikani aliko na kwamba bunge linalohodhiwa na upinzani litaanza mchakato wa kumuondowa madarakani.

Rais Rajoelina alitarajiwa baadae leo kulihutubia taifa kufuatia maandamano makubwa ya vijana wanaoungwa mkono na jeshi.