1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaJamhuri ya Kongo

Rais Denis Sassou Nguesso ashinda tena uchaguzi

18 Machi 2026

Rais wa Jamhuri ya Kongo-Brazaville Denis Sassou Nguesso ameshinda tena uchaguzi kwa asilimia 94.82 ya kura, na kuongeza awamu nyingine baada ya karibu miaka 42 ya kutawala taifa hilo.

https://p.dw.com/p/5AZxJ
Uturuki Ankara 2024 | Tume ya Uchumi kati ya Uturuki na Jamhuri ya Kongo-Brazzaville
Rais Denis-Christel Sassou Nguesso wa Kongo-Brazzaville ashinda awamu nyingine ya uchaguzi Picha: Muhammed Selim Korkutata/Anadolu/picture alliance

Wanadiplomasia na wachambuzi wa kisiasa walitarajia ushindi mwepesi kwa Sassou-Nguesso, 82, ambaye alikuwa akichuana na wapinzani sita ambao hawakuwa na umaarufu sana.

Wagombea walioshindwa wana siku tano za kuwasilisha pingamizi, na Mahakama ya Katiba ina siku 15 za kuchunguza changamoto zozote kabla ya kuchapisha matokeo ya mwisho.

Vyama vikuu vya upinzani havikuteua wagombea, wakilalamikia ukosefu wa uwazi, huku wapinzani wawili maarufu Jenerali Jean-Marie Michel Mokoko na Andre Okombi Salissa, wakisalia gerezani kwa karibu muongo mmoja.