SiasaJamhuri ya Kongo
Rais Denis Sassou Nguesso ashinda tena uchaguzi
18 Machi 2026
Matangazo
Wanadiplomasia na wachambuzi wa kisiasa walitarajia ushindi mwepesi kwa Sassou-Nguesso, 82, ambaye alikuwa akichuana na wapinzani sita ambao hawakuwa na umaarufu sana.
Wagombea walioshindwa wana siku tano za kuwasilisha pingamizi, na Mahakama ya Katiba ina siku 15 za kuchunguza changamoto zozote kabla ya kuchapisha matokeo ya mwisho.
Vyama vikuu vya upinzani havikuteua wagombea, wakilalamikia ukosefu wa uwazi, huku wapinzani wawili maarufu Jenerali Jean-Marie Michel Mokoko na Andre Okombi Salissa, wakisalia gerezani kwa karibu muongo mmoja.