1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa Leo XIV asafiri kuelekea Guinea ya Ikweta

21 Aprili 2026

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo XIV anasafiri Jumanne kuelekea Guinea ya Ikweta, kituo cha mwisho cha ziara yake ya siku 10 barani Afrika iliyomfikisha pia Algeria, Cameroon, Angola na Guinea ya Ikweta.

https://p.dw.com/p/5CYd2
Angola I Papa Leo XIV akisalimiana na bibi mmoja
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo XIV akisalimiana na bibi mmoja huko AngolaPicha: Vatican Media/Catholic Press Photo/IMAGO

Siku ya Jumatatu akiwa nchini Angola,  Papa Leo alilaani vitendo vya rushwa na unyonyaji unaofanywa na wenye nguvu dhidi ya wanyonge, na kwamba matumaini ya wengi yanakatishwa tamaa na ghasia zinazotumiwa ili kuwanufaisha matajiri.

Kiongozi huyo wa kiroho ametoa wito wa usambazaji wa haki wa rasilimali za Afrika akisema kuwa ukosefu wa haki unaharibu mioyo, huku mali za wengi zikimilikiwa na wachache.