1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Naqvi yuko Iran kwa mazungumzo ya kumaliza mkataba wa amani

20 Juni 2026

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Pakistan, Mohsin Naqvi, amewasili leo Iran kujadili kuendelea kwa mazungumzo na Marekani nchini Uswisi pamoja na uongozi wa Iran.

https://p.dw.com/p/5FlDA
Pakistan Lahore 2025 |Mohsin Naqvi akihutubia waandishi wa habari mjini Lahore mnamo Septemba 17, 2025
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Pakistan, Mohsin NaqviPicha: K.M. Chaudary/AP Photo/picture alliance

Kwa mujibu wa shirika la habari la Iran linalounga mkono serikali, Mehr, ndege ya Naqvi ilitua kwanza katika mji wa Mashhad ulio kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo, ambao ni kituo cha ziara za kidini.

Katika ziara yake, Naqvi anatarajiwa kukutana na viongozi wa timu ya mazungumzo ya Iran, spika wa bunge Mohammad Bagher Ghalibaf, pamoja na waziri wa mambo ya nje Abbas Araghchi.

Pakistan imekuwa mpatanishi rasmi kati ya pande zinazozozana za  Iran na Marekani tangu Aprili.

Washington na Tehran zilitia saini mapatano ya awali mwanzoni mwa wiki ambayo yanatarajiwa kukomesha uhasama katika eneo hilo na kurejeshwa kwa usafiri wa kibiashara kupitia Mlango-Bahari wa Hormuz.

Mazungumzo zaidi kuhusu masuala yenye utata, kama vile mpango wa nyuklia wa Iran, yanatarajiwa kuendelea ndani ya siku 60 zijazo.