1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MOSCOW : Watu 14 wauwawa huko Chechnya

20 Julai 2005
https://p.dw.com/p/CEss

Watu wasiopungua 14 wameuwawa na wengine 35 wakajeruhiwa katika shambulio la waasi katika jamhuri ya Chechnya. Motokaa ya polisi ililengwa kwa risasi na kulipuka katika mji mmoja kazkazini mwa mji mkuu Grozny.

Shambulio hilo limemlazimu rais Vladamir Putin wa Russia, kuuharakisha mpango wa kuifunga mipaka katika eneo la misukosuko la Caucasus. Maofisa wa Russia wanasema waasi wanapigana na wanajeshi wa Chechnya wanatumia maeneo ya milima ya Caucasus kukimbilia nchi jirani za Azerbaijan na Georgia.