Viongozi wa mataifa 20 yanayoongoza kiuchumi duniani wanakutana mjini Osaka Japan katika mkutano wa kilele wa G20 unaotarajiwa kuwa na mgawanyiko mkubwa. Mvutano kati ya Iran na Marekani pamoja na mgogoro wa kibiashara kati ya China na Marekani ni masuala yatakayotawala katika mkutano huo.