Maelfu wakusanyika kumkumbuka Benazir Bhutto nchini Pakistan
27 Desemba 2008Matangazo
Baadhi yao wakiwa wametembea kwa miguu kwa mamia ya maili kuweza kufika hapo.
Bhutto aliuwawa kwa kupigwa risasi katika shambulio la kujitolea muhanga kwa kujiripuwa wakati akiondoka kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni ya uchaguzi katika mji wa Rawalpindi nje kidogo ya mjii mkuu wa Islamabad hapo Desemba 27 mwaka 2007.
Mume wake Asif Ali Zardari alishika uongozi wa chama cha Bhutto baada ya kifo chake na alichaguliwa kuwa rais wa Pakistan hapo mwezi wa Septemba.
Waziri Mkuu Yousuf Raza Gilani amesema katika hotuba ya televisheni leo hii kwamba Bhutto aliwapa wananchi sauti na alikuwa ni matumaini ya wananchi wa Pakistan.
Umoja wa Mataifa umesema unataka kuchunguza kifo cha marehemu Bhutto.