1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ligi Kuu ya kandanda Misri kuanza tena

21 Machi 2015

Ligi kuu ya kandanda nchini Misri iliositishwa baada ya kiasi ya watu 19 kuuwawa katika mapigano baina ya mashabiki na na polisi kabla ya pambano la kandanda mwezi uliopita, itaanza tena Machi 30

https://p.dw.com/p/1Eusb
Ägypten Fußball fünf Tote bei Krawallen
Picha: Mohamed El-Shahed/AFP/Getty Images

Wengi walifariki kwa kukosa pumzi wakati umati ulikuwa ukikanyagana baada ya polisi kutumia hewa ya kutoa machozi kuwatawanya mashabiki walikuwa wakijaribu kuingia uwanjani kwa nguvu wakati wa pambano la Februari 8 kati ya Kilabu mbili zajiji la Cairo, Zamalek na ENPPI la mawaziri liliamua Jumatano na taarifa ikasema kwamba yatafikiwa makubaliano kati ya wizara ya vijana na michezo, wizara ya ndani, chama cha kandanda nchini humo na wapangaji ligi ili ianze mwisho wa mwezi huu kwa manufaa ya mchezo huo kwa Misri.

Mwandishi: Mohammed Abdul-Rahman, rtre, afp
Mhariri: Saumu Yusuf