Baraza la mawaziri nchini Kenya Alhamis lilitoa uamuzi wa kupiga marufuku hatua ya watoto wa Kenya kuasiliwa na raia wa kigeni. Mkutano huo maalumu uliofanyika jana ikulu mjini Nairobi, na kuongozwa na rais Uhuru Kenyatta uliitaka wizara ya kazi na ulinzi wa jamii kuunda sera mpya ya kusimamia suala hilo. sikiliza mahojiano kati ya Ysura Buwayhid na msemaji wa serikali Cyrus Oguna.?