Wakati teknolojia ikiendelea kukua na kuwanufaisha watu mbalimbali kote ulimwenguni, kuna ambao teknolojia hiyo hiyo imewaathiri na kuwaacha na huzuni kubwa na majuto. Nchini Marekani baadhi ya wazazi wameamua kuyashitaki makampuni makubwa ya teknolojia kutokana na athari za maudhui ya majukwaa ya makampuni hayo kwa watoto.