1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Indonesia yasema wanajeshi 8000 wako tayari kupelekwa Gaza

15 Februari 2026

Jeshi la Indonesia limesema leo kuwa takriban wanajeshi 8,000 wanatarajiwa kupelekwa katika Ukanda wa Gaza kama sehemu ya ujumbe wa kibinadamu na amani.

https://p.dw.com/p/58oFT
Uswisi, Davos 2026 |  Prabowo Subianto
Rais wa Insonesia Prabowo Subianto akitoa hotuba wakati wa Kongamano la Kimataifa la Uchumi DavosPicha: Cabinet Secretariat of The Republic of Indonesia

Kikosi cha jeshi la taifa la Indonesia, linalojulikana na kama TNI, kimekamilisha maandalizi ya vikosi vilivyopendekezwa pamoja na ratiba ya harakati zao kwenda Gaza ingawa bado serikali haijaamua ni lini wanajeshi hao watapelekwa. Haya ni kwa mujibu wa msemaji wa jeshi Brigedia Jenerali Donny Pramono.

Pramono ameliambia shirika la habari la Associated Press kwamba kimsingi, wako tayari kutumwa popote kwa notisi ya muda mfupi pindi serikali itakapoidhinisha rasmi.

Pia amesema, jeshi limetayarisha kikosi hicho cha takriban askari 8,000 kutokana na maamuzi yaliofanywa wakati wa mkutano wa Februari 12.