Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imewapiga marufuku raia kutembea ifikapo saa kumi na mbili jioni. Hatua hii inalenga kuwaepusha na mauwaji katika maeneo ya Beni mjini, Mavivi, Mbau, Oicha, Kokola, Mayimoya na Eringeti katika wilaya ya Beni. Hata hivyo hatua hiyo imepingwa na raia. John Kanyunyu alituletea ripoti hii kutoka Beni.