BiasharaChina
China yazibana kampuni za Japan, mvutano ukiongezeka
24 Februari 2026
Matangazo
Hatua hii ya leo Jumanne ya Beijing inaashiria kuongezeka kwa mvutano wa miezi kadhaa ulioongezeka baada ya Waziri Mkuu wa Japan Sanae Takaichi mnamo mwezi Novemba kusema kuwa Tokyo inaweza kutumia jeshi lake ikiwa kutakuwa na shambulizi dhidi ya Taiwan.
Wizara ya Biashara ya China imezizuia taasisi 20 za usafirishaji za Japan, baadhi zikiwa za kampuni ya Mitsubishi na shirika la anga za juu la Japan, ikiangazia suala la usalama wa taifa.
Wizara hiyo aidha imeongeza makampuni mengine 20 inayoendelea kuyafuatilia ni pamoja na ya kutengeneza magari ya Subaru ambayo bidhaa zake zinazosafirishwa nje zitakumbwa na ukaguzi mkali zaidi.