1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MichezoBrazil

Brazil yafuzu hatua ya mtoano ya 32 bora Kombe la Dunia

25 Juni 2026

Timu ya taifa ya Brazil imefuzu kwa hatua ya mtoano ya 32 bora baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3–0 dhidi ya Scotland katika mchezo wao wa mwisho wa Kundi C.

https://p.dw.com/p/5G2Sk
Kandanda | Michuano ya kufuzu Kombe la Dunia | Uruguay vs Brazil | Neymar
Mshambuliaji wa Brazil Neymar akikabiliana na kiungo Manuel Ugarte wa Uruguay kwenye uwanja wa Centenario huko Montevideo, Uruguay. Picha: Matilde Campodonico/AP Photo/picture alliance

Ushindi huo umeihakikishia Brazil nafasi ya kwanza kwenye kundi hilo, ikiwapiku Morocco kwa tofauti ya mabao, baada ya Morocco kushinda 4–2 dhidi ya Haiti mjini Atlanta.

Katika ushindi huo, mashabiki wa Brazil walipata habari njema baada ya Neymar, mshambuliaji mkongwe na mfungaji bora wa muda wote wa taifa hilo, kurejea uwanjani kwa mara ya kwanza kwenye michuano hiyo, akiingia katika kipindi cha pili na kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji.

Katika Kundi A, Afrika Kusini pia imefuzu hatua ya mtoano baada ya kuichapa Korea Kusini bao 1–0 mjini Monterrey na kumaliza katika nafasi ya pili.

Bafana Bafana sasa watakutana na Canada, ambao wameandika historia kwa kufuzu hatua ya mtoano kwa mara ya kwanza licha ya kupoteza 2–1 dhidi ya Uswisi mjini Vancouver.